Viwango vya ubora

Qualitätsstandards Foto: Goethe-Institut/ Sonja Tobias

Ubora. Neno tunalolipa uzito mkubwa

Katika taratibu zake za kusimamia ubora na miaka mingi ya uzoefu, Goethe-Institut inavuma kwenye utimizaji wa mahitaji makubwa yanayotarajiwa kutoka kwa watoaji wa mitihani ya lugha ya kigeni.

Mazoezi yametungwa na wataalamu wenye uzoefu wa kufundisha na utoaji wa mitihani na hupitia uhariri wa mwisho kwenye makao yetu makuu huko Munich. Kabla ya kutumika kwenye mitihani halisi, mazoezi hujaribiwa katika mazingira ya mtihani na matokeo hufanyiwa tathmini kwa vigezo vya ubora wake na idadi. Watahini hupokea mafunzo ya awali na mafunzo zaidi kupitia semina ambazo hufanyika kwenye makao yetu makuu na ofisi za kanda.

Viashiria vya ubora:

Upendeleo

Mitihani inapaswa kutoa haki kadri inavyowezekana kwa kila mmoja, bila ubaguzi wa jinsia, mbari au kilema chochote.

Uhalali

Lugha ya mitihani inapaswa kuzingatia tu uwezo katika isimu na siyo uwezo wa mtahiniwa wa kukariri, akili au maarifa ya ulimwengu.

Uaminifu

Kiwango cha juu cha uaminifu kimehakikishwa kwa kila mtihani kusahihisha na watahini wawili.

Utumikaji

Tunafanya kazi bila kuchoka kuendeleza mitihani yetu kwa kuboresha muda wake, kwa kutumia teknolojia ya kisasa na kutengeneza mazingira bora zaidi ya mtihani.

Kigezo cha ubora wa kiwango:

Kama mwanachama mwanzilishi wa Ushirika wa Watoaji wa Majaribio ya Lugha - Ulaya (ALTE) tunapigania the maendeleo na utekelezaji wa viwango vya ubora.
 
ALTE imejiwekea malengo yafuatayo:
  • kusanifisha ngazi za uwezo ili kuchochea kutambuliwa kimataifa kwa vyeti vya lugha barani Ulaya;
  • kusanifisha vigezo vya ubora for all the hatua zinazohusika kwenye maandalizi na mchakato wa mitihani, mf. usanifu na uchapaji wa majaribio, utoaji wa mitihani, upimaji, uthibitishaji, ufanyaji wa tathmini na uhifadhi wa data;
  • ushirikiano katika miradi ya pamoja na kubadilishana uzoefu na  maarifa ya kitaalamu.
Mwaka 2003, ALTE ilipokelewa kwenye Baraza la Ulaya kama asasi ya kiraia (NGO) na tangu wakati huo imekuwa inatoa ushauri wa msingi juu ya mada kama vile upimaji wa utendaji na uthibitishaji. Mwaka 2006, ALTE ilipewa hadhi maalumu ya uangalizi kwenye Umoja wa Mataifa.
Juu