"Shule: Washirika kwa ajili ya siku zijazo" (PASCH)

  • Initiative „Schulen: Partner der Zukunft“ © Kai Uwe Oesterhellweg

  • Initiative „Schulen: Partner der Zukunft“ © Kai Uwe Oesterhellweg

  • Initiative „Schulen: Partner der Zukunft“ © PASCH-net

  • Initiative „Schulen: Partner der Zukunft“ © Kai Uwe Oesterhellweg

  • Initiative „Schulen: Partner der Zukunft“ © Keller

  • Initiative „Schulen: Partner der Zukunft“ © PASCH-net

  • Initiative „Schulen: Partner der Zukunft“ © Jens Sauerbrey

Mradi wa "Shule: Washirika kwa ajili ya siku zijazo" (PASCH) unatengeneza mtandao wa kimataifa wa zaidi ya shule 2,000 zilizo na uhusiano mahsusi na Ujerumani. Goethe-Institut inatoa msaada kwa takribani shule 600 za PASCH katika mfumo wa elimu ya taifa kutoka zaidi ya nchi 100.

Mradi wa "Shule: Washirika kwa ajili ya siku zijazo" (PASCH) ulizinduliwa Februari 2008 na Wizara ya Mambo ya Nje ya Ujerumani. Mradi wa PASCH unaratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na unatekelezwa kwa ushirikiano na Wakala Mkuu wa Shule za Nje (ZfA), Goethe-Institut, Ofisi ya Ushirikiano wa Kitaaluma ya Ujerumani na Ofisi ya Ushirikiano wa Kitaaluma ya Kamati ya Kudumu ya Wizara ya Elimu na Mambo ya Utamaduni ya Länder ya Jamhuri ya Shikisho la Ujerumani.

Kanuni na malengo

PASCH inaratibiwa kulingana na kanuni kuu nne:
  • kufikia matarajio kupitia elimu
  • kukuza uelewa kupitia lugha mbalimbali
  • kujifunza lugha na kupata elimu na
  • kukabili pamoja matatizo yajayo kama jumuiya ya wasomi kimataifa

Juu