
Utafiti wa tathmini ya mpito wa kozi ya lugha kabla ya shirikishi kwenda kozi shirikishi ( 2011) ilionyesha kuwa wahamiaji wapya ambao wamefaulu tayari mtihani wa A1 kwa ajili ya viza kwenye nchi zao , wanatakiwa kusubiri muda mrefu mpaka wajithatiti kwenye lugha ya kijerumani na utamaduni kwa mara nyingine kwenye kozi shirikishi. Kwa kuongezea , katika utafiti huu pia ilionyesha kuwa kuna upungufu mkubwa wa usomaji, mazoezi na nyenzo za taarifa zilizotengwa kwa ajili ya kundi hili lengwa na mahitaji ya wanafunzi, ambayo kwayo wanaweza kuendelea kujifunza binafsi wakati wa kipindi cha mpito. Kutokana na upungufu huu wa nyenzo, wakati wahamiaji wanajiunga na kozi shirikishi, ujuzi wao wa lugha mara nyingi unafifia. Hata hivyo-kwa mujibu wa wahamiaji-kuna kiwango kikubwa cha hamasa ya kuendelea kujisomea.
Zur Studie „Der Übergang von der vorintegrativen Sprachförderung zum Integrationskurs“
Goethe-Institut inakabiliana na hitaji hili kwa kuwa na saiti ya mtandao “ Mein Weg nach Deutschland”, kuendeleza na kuchochea ufundisha wa lugha mpito wa kabla ya shirikisho kwenda kozi ya shirikishi” , mradi ambao umefadhiliwa kwa pamoja na mfuko kutoka shirikisho la mfuko ulaya EIF.
Mradi unalenga kuboresha mpito kati ya ujifunzaji wa lugha kabla ya shirikishi, taarifa na kozi za ushauri za nje ya nchi na ufundishaji wa mwanzo wa lugha , pia ufumbuzi wa shirikisho uliotolewa na serikali shirikishi nchini Ujerumani. Kufanikisha hili, saiti ya mtandao itaboresha na kuimarisha ujuzi wa mwelekeo uliokwisha fahamika kupitia masomo shirikishi kabla ya shirikishi. Zaidi, kwa kutumia nyenzo zinazopatikana kutoka saiti hii itasaidia kundi hili lengwa la wanafunzi kujifunza ujunzi mbalimbali kwa ajili ya kuishi Ujerumani-kama vile namna gani ya kujishulisha na aina kadhaa za vyombo vya habari, ujuzi wa mwelekeo wa muda wa mwanzo nchini Ujerumani.
Kwa kubonyeza tabu ya “Kwa walimu” , walimu na washauri wa uhamiaji wanaweza kupata taarifa ya filamu ya dakika 5 kuhusu tovuti, pia karibu kurasa 30 katika nyaraka za pdf ambazo zinatoa mwongozo juu ya utumizi wa wa mtandao kwa madarasa.
Katika ncha hii tungependa kuwashukuru kwa dhati waandishi wote , waendelezaji, watengenezaji wa filamu, watengenezaji wa vielelezo, wahariri na wataalamu ambao wamehusika katika mradi huu, na michango yao imehakikisha kwamba saiti hii ikiwa na maudhui ya kitaarifa tofauti tofauti, ambayo yanapatikana mtandaoni! Kwa mantiki hii, wametajwa kwa majina katika kurasa za “Kufanya mazozezi ya kijerumani”. Tungependa pia kuwashukuru waandishi na wahariri Stefan Münchow, Freya Conesa, Joanna Chlebnikow, Csaba Gloner, Janna Degener, Ellen Bachmann na Marion Hollerung kwa kuandika na kuhariri mazoezi muhimu na makala ya saiti ya mtandao.
Zaidi ya hayo, tunatoa shukrani zetu kwa umoja wa ulaya, bila ya ufadhili huu isingewezekana kutekeleza mradi huu kwa msaada wake wa kifedha