Ndoa
Katika nchi nyingi waja hufunga ndoa katika Mamlaka ya usajili wa ndoa. Hii ni ndoa inayotambuliwa na serikali. Hali ni vivyo hivyo nchini Ujerumani. Ni kwa njia hii tu ndoa inakuwa halali. Baada ya hapo, mja anaweza pia kufunga ndoa ya kanisa. Ili kufunga ndoa, wote wawili sharti wawe na angalau umri wa miaka 18.