Kufundisha Kijerumani
Dhamira ya Goethe-Institut ni kukuza utamaduni wa Kijerumani na kuendeleza ufundishaji na ujifunzaji wa Kijerumani kama lugha ya kigeni. Tumejitolea kutoa mafunzo ya hali ya juu ya maendeleo ya kitaaluma kwa walimu na vifaa vya kufundishia bila malipo ili kufanya kujifunza Kijerumani kuwa jambo la kufurahisha na rahisi.
Mawasiliano
Ushirikiano wa Kijerumani kama Lugha ya Kigeni unasaidia walimu wa Kitanzania, shule na taasisi katika kufanikisha ufundishaji wa lugha ya Kijerumani. Tunatoa mafunzo kwa walimu wa Kijerumani, kuanzia warsha za siku moja hadi semina za wiki kadhaa. Pia tunatoa mawazo na vitendea kazi vya kuhamasisha ujifunzaji wa Kijerumani pamoja na muhtasari wa vifaa vya kisasa vya kufundishia.